Tuesday, April 8, 2014

UJAUZITO WA MIEZI KUMI NA MBILI NA KUZAA MTOTO WA AJABU - PATA USHUHUDA WAKE

===================THIS IS MY STORY=============
JUMAPILI 06 April, 2014...... (Ufufuo na Uzima - Morogoro)
USHUHUDA WA LEO: THIS IS MY STORY, BY CESILIA (Part One)
Utangulizi: Cesilia Alilkuwa ameolewa Tanga na mwanaume ambaye alikuwa mganga wa kienyeji, ila hakuwahi kumweleza ukweli kuwa ni mganga. Alipata ujauzito uliodumu kwa miezi 12 na kisha akaamua kwenda kwa mganga wa kienyeji kuaguliwa. Mganga akamwambia anatakiwa apatiwe dawa ya kuishusha nyota yake. Alimletea dawa ambayo ni mavi ya tembo, ambayo alitakiwa akoroge hiyo dawa nyakati za saa nane usiku ainywe. Alitakiwa atumie sumaku kuishusha hiyo dawa kuanzia kifuani hadi tumboni ili hapo kesho yake aweze kujifungua. Hata hivyo ilipofika kesho yake hakujifungua.

Wengine walimwambia aende kwa bibi yake kijijini. Bibi huyo alimpeleka kwa mkunga. Mkunga alimwambia inaelekea hiyo mimba ni kubwa sana, ila anachotakiwa ni kuwa akipata tu uchungu aende hospitali. Cesilia aligoma kwenda hospitali akisema “kama ni kufa na nife tu”, haya aliyasema akiwa nyumbani kwake.
Siku ya siku ililazimu kwenda hospitalini, ambapo walimwambia inaelekea ana mimba ya Watoto wanne. Hata hivyo hospitalini pale manesi walikuwa wananong’onezana wao kwa wao kwamba huyu mgonjwa ni wa kufa, na hakuna uwezekano wa kupona. Pale hospitalini madktari waliitana na kumwambia asaini hati ya kufanyiwa operesheni. Wakati wa kufanyiwa ile operesheni, ghafla alikosa fahamu, kisha akajikuta yupo mahali ambapo wamejaa Waarabu, na walikuwa wanachezea midoli. Waarabu hawa Walikuwa wakimlazimisha apokee hiyo midoli, lakini akakataa. Baada ya kuzinduka usingizini, alimkuta mdogo wake pembeni mwa kitanda. Alimuuliza dada yake kipi kinaendelea akaambiwa, tayari ameshafanyiwa operesheni na mtoto wako yupo kwa manesi. Aliomba kupatiwa mtoto amuone, lakini alipoletewa kumuona, alishangaa kumuona mtoto wake kuwa na kichwa kikubwa sana. Mtoto huyu alikuwa mlemavu kiasi kwamba hawezi kugeuza kichwa chake.

Ndani ya Mwezi mmoja wa kuishi kwa yule mtoto tayari alikuwa na uwezo wa kuongea maneno kama ‘mama hamna, baba, babu’….. Huyu mtoto nyakati nyingine alikuwa na vituko kiasi kwamba majirani wa kiislamu walikuwa wanamtia moyo mama huyu, eti katika dini yao Watoto kama hao wapo, na ni maalumu kwa kutoa shuhuda. Pamoja na kwamba mtoto huyu alikuwa hawezi kujiegeuza, lakini nyakati za usiku mama yake alikuwa akiamka anamkuta huyu mtoto akiwa kwenye titi ananyonya, na akawa anajiuliza ni nani anayemsaidia kumweka mtoto kwenye titi bila kupata majibu.......!!!!

Siku moja alitokewa na majini matano. Hawa walikuwa wamevaa baibui, wakamtishia wakisema, “wewe ni wifi yetu, uliolewa na kaka yetu, na sasa hutaki kumleaa huyu mtoto. Kuna siku tutakuja kumchukua huyu mtoto, tutakupa pesa, na ukifanya mchezo tutaondoka na wewe pia ili ukamlee huyu mtoto”. Walimpa Tarehe na muda wa kuja kumchukua huyu mtoto. Siku tatu kabla ya Tarehe majini waliyosema ni ya kumchukua mtoto huyu, alipata wazo la kuchangisha michango akitumia picha ya yule mtoto ili mtoto akapatiwe matibabu ya kichwa chake. Waliomshauri walimwambia apite kwenye maduka ya WAARABU na WAHINDI kwani ni wazuri sana kwenye kuchangia mambo kama haya, naye akafanya hivyo.

Mama alivyorudi aliambiwa mwanao amekunywa maziwa kikombe lakini papo hapo akatapika puani mitihili ya maji maji. Mama alimuitaa mwanae kwa jina lake la Robert, naye akamuitikia mama yake, huku akimpangusa machozi mama yake. Hata hivyo alikufa baadae kidogo na kupelekwa kijijini kwa mazishi, wakitumia pesa ile ya michango ya jana yake, sawasawa na lile neno aliloambiwa na yale majini kuwa watampatia pesa. Walifanya mazishi ya haraka haraka nyakati za usiku kwani waliokuja pale walishauri maiti asikae muda mrefu kwani alikuwa anaumuka na kuongezeka umbile lake. Bwana wake alikasirika sana mwanae huyu kuzikwa mahali nje ya Njombe kwani alikuwa ni mzaliwa wake wa kwanza.

Bwana wake alianza kujidhihirisha kuwa ni mganga kweli kweli. Aliamua kumpeleka mke wake huyu Ukerewe ili apewe cheo kikuu cha kufanya uganga. Mashekhe walimlazimisha mama huyu abadili dini lakini akagoma. Baadaye walifanya dawa zao ambazo zilileta kizazaa kwa mtoto mwingine wa mama huyu aliyemzaa na mume mwingine kabla ya kuanza mahusiano na bwana huyu mganga. Hata hivyo bwana huyu alimpa dawa/mitishamba mtoto huyu wa kambo na akapona.

Baadaye bwana huyu alihamia Kiteto, kijiji cha Dosidosi ambako alimuita mke wake wakae pamoja ili amsaidie kwenye kazi ya kuvuta wateja. Huyu mama alimfuata, na kisha akawa na kazi ya kuandika maneno yote ya kiaguzi / kiganga pindi wateja wanapokuja kufanyiwa uganga. Miongoni mwa dawa za mganga huyu ni unyayo wa bata na kiini cha yai la bata. Kwa hiyo maisha ya kula kuku-nyama yakamfurahisha sana huyu mama, na kujiona yupo salama. Baadae siku moja baada ya kufanyiwa uganga usiku, ndipo tatizo la kutokwa damu mfululizo likamuanza huyu mama.

Alipoona hali yake ya kutokwa na damu inaendelea kumsumbua, alienda Hospitalini ambapo alipata vipimo vyote, na kukutwa na magonjwa mengi tu kama vile typhoid, Ukimwi, malaria kali, ukosefu wa damu n.k. Siku ya 69 baada ya damu mfululizo kuendelea kumtoka huyu mama, aliletwa hapa kanisani (UFUFUO NA UZIMA – MOROGORO) kuombewa, baaada ya kupewa ushauri huu na baba mdogo wake anayeitwa Amani. Baada ya Maombi, damu yake ilifunga papo hapo. Bwana wake alipiga simu siku hiyo hiyo akilaumu kwa nini amepelekwa kanisani badala ya kupelekwa kwa mashekhe wawili kufanyiwa tiba mbadala. Usiku wake huyu mama aliota ndoto kuwa amekutanishwa na babu yake ambaye ni marehemu. Bwana wake akawa anampigia simu mkewe huyu kusema, amemvurugia mambo yake. Mongoni mwa shutuma nyingine ni kuwa, balaa zilikuwa zinaikumba sana familia ya huyu bwana, ikiwemo ajali za pikipiki na moto kwa ndugu zake. Nyakati nyingine alimpigia simu mkewe kumwambia eti Maombi ya Wakristo ni sawa na uchawi.
==USHUHUDA HUU SEHEMU YA PILI UTAENDELEA WIKI IJAYO==

==Na Mwandishi Wetu==
== Information Ministry (Ufufuo Na Uzima - Morogoro)==
PICHANI: Cesilia akielezeea ushuhuda wake (part one) katika Nyumba ya Ufufuo na Uzima - Morogoro Jumapili 06 April 2014. Kushoto kwake ni AP Steven Nampunju na Kulia ni SNP (Baba) Godson Issa Zacharia wa Ufufuo na Uzima - Morogoro