Moshi yote kwa YESU! Hata aliyekuwa
mtoni sauti ya njoo imemfikia.GUDIRA JOSEPH MUSHI, ameisikia sauti ya njoo leo akiwa
mto Rau ulioko mjini Moshi, yaliyokuwa makao yake. Binti huyu leo amerudishwa
toka msukuleni nakueleza alivyo kuwa akisababisha ajari na kusimamisha magari
katika eneol a mto RAU.Gudira alionekana kupigwa na butwaa huku akishangaa
mazingira ya kusanyiko la watu wengi,wakati anadai kuwa amezoa kuishi majini,
huku viumbe vya majini vikiwa ndo marafiki zake. Asifiwe Mungu wa wote wenye
mwili aliye mtoa katika makao ya kuzimu.
MCHUNGAJI KAPANGE
Mchungaji Kapange, wa mjini moshi baada ya kutoka kwenye mkutano wa Mch.Kiongozi josephat Gwajima, na kuona jinsi watu maelfu kwa maelfu wanavyo rudishwa kutoka katika vifungo vya shetani kwa kuitwa njoo na kuitiwa kwa Jina la Yesu, aliona ni vyema akajaribu kuyatumia maarifa na mamlaka hayo nyumbani kwake kwa mwane wa kike aitwaye Herrith.
Baada
ya kumuita kwa muda kidogo tu, mtoto akashtuka kwa nguvu sana, na
kuanza kumuhoji baba yake ambaye ndiye mchungaji aliyeyabeba maarifa
hayo kutoka mkutanoni, na kumuuliza hapa ni wapi baba?, mbona mimi skua
hapa...
ndipo
Mchungaji kapange alipo amua kukoleza moto na kumrudisha mtoto wake vizuri
na baada ya hapo akamuweka ufahamu wake sawa kwa kumuombea tena kwa Jina
la Yesu,na kumuwekea ulinzi wa Damu ya Yesu, ndipo mtoto alipoanza
kutoa ushuhuda wake kuwa alikuwa anaishi kuzimu, na dude linaloaminika
kuwa ni shetani aitwaye, mkuu wa kafara pia baba yake akamuuliza kwa nini kila siku nilipokuwa nakuuliza kama unashida yoyote hukuwa unasema? , mtoto akajibu kuwa alikuwa amefungwa na haoni na wala hawezi kusema, na alipohojiwa na Mchungaji
Kiongozi Josephat Gwajima wakati akitoa ushuhuda wake mbele ya mkutano
alidai kuwa alikuwa amechukuliwa na mtu anayeitwa KANUMBA...na uwanja
mzima ukalipuka kwa mshangao
"Na ndio maana kama kuna wakuchukia Duniani, ambaye anatakiwa abezwe na watu wote ni mchawi anaye "m-host" shetani - -Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima
|