Friday, October 25, 2013

ALIYEKUWA AMEPOTEA KWA MIAKA MINNE APATIKANA BAADA YA MAOMBEZI MKUTANO WA Mch. Josephat Gwajima - Moshi..


   Mama mmoja mkazi wa Moshi, apokea muujiza wake wa kumpata mwanae aliyefahamika kwa jina la YONA HONEST aliyekuwa amepotea katika mazingira ya kutatanisha kwa kipindi cha miaka 4 iliyopita. Mama huyu mara baada wa kuhudhuria mkutano kwa mara ya kwanza, aliamua kuchukua hatua ya kuandika
 
Jina la mwanae aliyekuwa amepotea. Mshangao ulitokea pale kijana huyu alipokuwa anaelezea kuwa alikuwa amewekwa mateka huko mkoani Tanga, huku mama Yona anashuhudia kuwa  baada ya kufika kwenye mkutano Yona amepatika Mkoani Dodoma na kuweka kwenye box. Mama YONA akiwa katika hali ya furaha huku akimtazama kijana wake alimshukuru sana Mungu kwa kumrudisha mtoto wake, aliyedai kupotelea Tanga huku akifanyishwa kazi ya kukamua ng’ombe aa watu maziwa kwa kipindi chote hicho. 
BINTI MARY KISIMBO


Binti huyu anaitwa Mary Kisimbo anatoa ushuhuda wake kuwa alikuwa amewekwa makaburini, na bibi mmoja ambaye hamfahamu vizuri,lakini ni mweusi sana.Baada ya maombezi ya Mch. kiongozi Josephat Gwajima,  Anadai alianza kuisikia sauti inamuita njoo kwa jina la Yesu na akashtukia yuko uwanja wa mashujaa. Binti huyu alimshukuru Bwana Yesu kwa kumuweka huru kutoka kwenye kifungo hicho cha shetani na akaahaidi kumkabidhi Mungu maisha yake na kumtumikia.




   Baada ya kuvunja laana za familia, JANETH SHIRIMA aliyechukuliwa katika mazingira ya kichawi na kuishi Mombasa, aliachiwa huru na waliomchukua wakidai kuwa hafai, !! 
Mwana mama huyu alisema kuwa baada ya mchungaji kuomba juu ya mji wa moshi huku akitamka “moshi na mitaa yake, moshi na laana zake, moshi na watu wake “njooooo” sauti hii ilisikika katika sahemu alikokuwa binti  huyu ameshikiliwa na wakamtupa wakmuachia . JANETH anashuhudia kuwa jumla ya mabinti 10,000 wenye umri mdogo  aliwachukua na kuwafanya machangudoa (wakiuza miili yao). Janeth alisisitiza kwa sauti ya hasira kuwa wachawi wa pigweeee kwa JINA LA YESU.
 AMINA SELEMANI

Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima akimuombea binti huyu anayeitwa Amina Selemani, ambaye alikuwa amefichwa kishirikina kwenye mashamba huko mkoani Tanga, likuwa akilishwa nyama za watu, na kulazimishwa kushiriki mambo ya kichawi baada ya maombezi ya Mch.Gwajima aliskia sauti inamuita njoo kwa jina la Yesu alikuja na usafiri wa ungo ambao kuna watu walikuwa wamembeba na kummbwaga.
 GLORY SHAYO
Binti huyu anaitwa Glory Shayo, anaelezea kisa chake, kuwa, siku moja alikuwa shule ghafla akazimia kwenye mida ya saa saba, lakini baada ya muda mchache akazinduka, half saa nane tena akazimia , akaamka yuko hopitali ya St.Joseph lakini akaambiwa hana ugojwa ,ila ndio ukawa mwanzo wa kuanza kushambuliwa mara kwa mara na magonjwa mbalimbali ambayo hakuna hospitali inayompa maelezo mazuri ni ugonjwa gani hasa unaomsumbua, baada ya kufika kwenye mkutano, na kufuata maombezi ya mchungaji josephat Gwajim, kuwa kila mtu uwanjani asemae anaomba kumuona yule mtu muovu anaye lta uadui katika masiha yake ndio ghafla akashtukia chini na akmuona aliyekuwa akimtesa, kumbe ni mtu wake wa karibu, aliyekuwa amedhamiria kumfanya ashindwe kabisa kusoma shuke, ambaye aliweza kumtaj kwa jina moja tu kuwa ni Halima,


Mchungaji Kiongozi wa kanisa la ufufuo na uzima akistaajabishwa na habari za Binti huyu ambaye, analezea mbele ya watu kuwa alikuwa nchini Congo alikopelekwa na bibi yake,ambako alikuwa amechukuliwa kiuchawi na kuwa msukule katika nchi hiyo ya Congo na kazi yake kubwa ilikuwa ni kuuwa watu kwa njia za uchawi,ila baada ya maombezi ya Mch. Kiongozi Josephat Gwajima alisikia sauti inamwuta njoo na ghafla akaletwa na aliyemchukua kwa kutumia usafiri wa kichwa cha mtu.
 GUDIRA JOSEPH MUSHI


  Moshi yote kwa YESU! Hata aliyekuwa mtoni sauti ya njoo imemfikia.GUDIRA JOSEPH MUSHI, ameisikia sauti ya njoo leo akiwa mto Rau ulioko mjini Moshi, yaliyokuwa makao yake. Binti huyu leo amerudishwa toka msukuleni nakueleza alivyo kuwa akisababisha ajari na kusimamisha magari katika eneol a mto RAU.Gudira alionekana kupigwa na butwaa huku akishangaa mazingira ya kusanyiko la watu wengi,wakati anadai kuwa amezoa kuishi majini, huku viumbe vya majini vikiwa ndo marafiki zake. Asifiwe Mungu wa wote wenye mwili aliye mtoa katika makao ya kuzimu.


MCHUNGAJI KAPANGE

    Mchungaji Kapange, wa mjini moshi baada ya kutoka kwenye mkutano wa Mch.Kiongozi josephat Gwajima, na kuona jinsi watu maelfu kwa maelfu wanavyo rudishwa kutoka katika vifungo vya shetani kwa kuitwa njoo na kuitiwa kwa Jina la Yesu, aliona ni vyema akajaribu kuyatumia maarifa na mamlaka hayo nyumbani kwake kwa mwane wa kike aitwaye Herrith.

Baada ya kumuita kwa muda kidogo tu, mtoto akashtuka kwa nguvu sana, na kuanza kumuhoji baba yake ambaye ndiye mchungaji aliyeyabeba maarifa hayo kutoka mkutanoni, na kumuuliza hapa ni wapi baba?, mbona mimi skua hapa...
ndipo Mchungaji kapange alipo amua kukoleza moto na kumrudisha mtoto wake vizuri na baada ya hapo akamuweka ufahamu wake sawa kwa kumuombea tena kwa Jina la Yesu,na kumuwekea ulinzi wa Damu ya Yesu, ndipo mtoto alipoanza kutoa ushuhuda wake kuwa alikuwa anaishi kuzimu, na dude linaloaminika kuwa ni shetani aitwaye, mkuu wa kafara pia baba yake akamuuliza kwa nini kila siku nilipokuwa nakuuliza kama unashida yoyote hukuwa unasema? , mtoto akajibu kuwa alikuwa amefungwa na haoni na wala hawezi kusema, na alipohojiwa na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima wakati akitoa ushuhuda wake mbele ya mkutano alidai kuwa alikuwa amechukuliwa na mtu anayeitwa KANUMBA...na uwanja mzima ukalipuka kwa mshangao

"Na ndio maana kama kuna wakuchukia Duniani, ambaye anatakiwa abezwe na watu wote ni mchawi anaye "m-host"  shetani - -Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima akiwa katika picha ya pamoja, na baadhi ya waliofika mkutanoni na kupokea miujiza yao na kuwekwa huru kutoka kwenye vifungo mbalimbali vya shetani hasa hasa ilikuwa ni siku ya kuzivunja laana za familia, na kuwaweka huru ambao walikuwa wako msukuleni. Nyuma ya mchungaji kiongozi ni Mchungaji Mwandamizi Mkuu (SRP) Grace Gwajima na aliyevalia kofia ya kiaskari ni Mchungaji Mwandamizi (RP) Maxmillian Machumu.

No comments:

Post a Comment